May 24, 2013

Nape akaribishwa Berlin Ujerumani

 Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, CCM, Nape Nnauye (katikati) akikaribishwa na baadhi ya viongozi wa chama cha SPD mjini Berlin, Ujerumani alipowasili jana kuhudhuria sherehe za miaka 150 ya kuzaliwa kwa chama hicho cha SPD.

Rais Kikwete aipa tuzo PSPF

 
 Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi  Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa PSPF Ndugu. Adam H. Mayingu  tuzo ya kuwa Mfuko wa kwanza wa Hifadhi ya Jamii Tanzania kutoa mikopo ya nyumba kwa wanachama wake.  Tuzo hiyo ilitolewa kwenye maadhimisho ya kilele cha Wiki ya Mifuko ya Jamii mjini Dodoma.  Mh. Raisi alisema PSPF ni mfuko madhubuti na una fursa nyingi za kimaendeleo kwa wananchi wa Tanzaniai na unauwezo mkubwa na salama katika uwekezaji . 

Aliongezea kwa kusema sio kweli kwamba Mfuko huu uko mahututi kama ilivyozungumziwa kwenye baadhi ya vyombo vya habari, bali Mfuko huu unadai wadai wake Trilioni 6 na kudai sio kufilisika tena

Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Jakaya Mrisho Kikwete akisoma kipeperushi cha nyumba za PSPF zinazokopeshwa kwa wanachama wa Mfuko huo, huku akimsikiliza Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa  Mfuko huo ndugu Adam H. Mayingu akimuelezea kuhusu nyumba hizo na fursa zingine zilizopo PSPF kwa Watanzania ikiwa ni pamoja na ujumbe kwa Watanzania kwamba mtu yeyote mwenye umri usiopungua miaka 18 anaweza kuwa mwanachama wa PSPF

  Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF ndugu Adam H. Mayingu akimuelezea Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dr. Rehema J. Nchimbi kuhusu shughuli za Mfuko na fursa zilizopo kwa watanzania hususani mikopo ya nyumba na mafao ya aina mbalimbali ikiwemo fao la Ujasiliamali na Elimu.
   Mtangazaji wa TBC Amina Mollel akikabidhi fomu ya kujiunga na PSPF kwa Meneja Masoko wa Mfuko huo Bi. Costantina Martin mala baada ya kuvutiwa na kukata shauri ya kuwa mwanachama wa Mfuko wa kwa njia ya uchangiaji wa hiari
 Timu ya PSPF iliyokuwa kwenye maonyesho ya wiki ya hifadhi ya Jamii wakiwa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wao ndugu Adamu Mayingu katikati.  Timu hiyo inastahili pongezi kutokana na uduma bora waliyokuwa wakiitoa kwa wananchi waliokuwa wakitembelea banda hilo la PSPF pale Nyerere squire Dodoma.
Wanachama wa PSPF wakipata taarifa mbalimbali ikiwapo historia ya michango yao na taarifa za uanachama.


May 22, 2013

MAONI YA CARTHBERT KAJUNA KUHUSU TAALUMA YA UANDISHI WA HABARI NDANI YA MAGAZETI TANDO/MITANDAO YA KIJAMII

Kajunason
Watu wengi kwa sasa wameibuka na kutokea kuipenda fani ya uandishi wa habari bila kujua misingi na miiko ya uandishi wa habari. Tatizo moja ambalo limeonekana ni kubwa sana ni utandawazi ambao umekuwepo na kutokea ibuko la kila kijana kufungua gazeti tando (blog).

Hatukatai kuja kwa magazeti tando ila naomba tujiulize, yanatumika ipasavyo ama ndiyo limekuwa ni wimbi vamizi lenye kutoa ama kusambaza habari hata zile zisizokuwa na vyanzo kamili na visivyojitosheleza.Kwa sasa imezuka tabia ya wanaojiita wamiliki wa magazeti tando,wengi wao kukopi na kupaste vitu wanavyoviokota katika mitandao ya kijamii ikiwemo Twitter, facebook na mingine mingi.

Sina nia ya kumsema mtu bali napenda tuelimishane kama vijana wenzangu,ambao wametokea kuipenda fani ya uandishi wa habari, wakumbuke kuwa fani ya uandishi wa habari ina miiko na maadili yake, mfano. Katika kuandika habari za mazingira, siasa, elimu, uchumi, michezo, burudani ukiangalia habari hizi zote zina misingi na miiko yake.

 Leo hauwezi kumchukua mwandishi wa habari za michezo ukamwambia aandike habari za uchumi kwa vile hatakuwa na takwimu za uchumi na hata akiandika hiyo habari na ukiisoma utakuwa unajiuliza maswali mengi bila kupata majibu.

Vile vile ni vizuri vijana wenzangu kutambua kuwa kila kazi ina mipaka na misingi yake, juzi juzi nilisoma habari katika gazeti tando moja wapo ikisema, ‘ALIYEONGOZA MAANDAMANO YA IRINGA MHESHIMIWA MCHUNGAJI MSIGWA ASWEKWA NDANI’ nilijiuliza maswali mengi ambayo kiukweli nilikosa majibu yake, kuona huyu aliyeandika hiki kichwa cha habari kweli amepitia fani ya uandishi wa habari ama ndio ule upepo vamizi?

Maana unapoandika habari za mahakamani, polisi kuna misemo yake, hauwezi kumuhukumu mtu moja kwa moja kwa kusema fulani ni mwizi, hata hao polisi ambao huwa wanakwenda kukamata watu eneo la tukio hawawezi kusema fulani ni mwizi mpaka apelekwe mahakamani ndipo sheria ichukue mkondo wake na kumbaini huyo aliyekamatwa ni mwizi.

Naomba tufike mahali tuheshimu utu wa watu na kuepuka udhalilishaji wa bila kujua naamini baadhi ya vijana wengi walioamua kufungua magazeti hayo tando ambayo yanatoa habari, hawana taaluma ya uandishi wa habari.

Napenda kuwapongeza wale walioamua kufungua magazeti tando katika milengo yao tofauti ikiwemo kutoa habari kwa njia ya ‘kufundisha masuala ya urembo, mapishi, kuwasaidia kuwatangaza vijana katika muziki na hata wale walioamua kuandika habari zao binafsi.

Nayasema yote hayo kwa vile kumezuka wimbi la vijana wanaotaka kuichafua fani ya uandishi wa habari na ionekane si fani ya watu walioenda shule bali ni ya wahuni tu wasiojua mambo, naomba vijana tuelimike na tujifunze kwa watu wanayoyajua mambo ili tuweze kufika mbele zaidi.

Namalizia kwa kusema tusipoziba ufa tutajenga ukuta.

Asanteni sana kwa kusoma.

Imeandikwa na Cathbert A. Kajuna

www.kajunason.blogspot.com

May 21, 2013

VITUKO MITAANI

Umetoka kwenda town kwenye mishemishe zako umemuachia dada wa kazi maagizo afanye usafi vitu vyako vyote chumbani. Unarudi unakuta kazi hii hapa.


Mama Salma Kikwete akutana na Daktari Bingwa wa Watoto kutoka Marekani, Jerome Paulson

Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) na Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akimkaribisha kwa mazungumzo Daktari bingwa wa watoto Jerome Paulson, Mkurugenzi wa Afya ya watoto na Mazingira kutoka Chidren's National Medical Center ya huko Washington nchini Marekani aliyemtembelea Mama Salma kwenye ofisi ya WAMA jijini Dar es Salaam tarehe 21.5.2013. Dr. Jerome amekuja Tanzania kwa ajili ya kutoa mafunzo kwa Madaktari Bingwa wa watoto hapa nchini kuhusu afya ya mtoto na mazingira  kufuatia makubaliano aliyoyafanya na Mama Salma wakati alipotembelea taasisi hiyo huko Washington mwaka 2012.

Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akipokea zawadi ya picha kutoka kwa Daktari Bingwa wa watoto Jerome Paulson aliyeambatana na Mkewe pamoja na viongozi wa Chama cha Madaktari wa watoto hapa Tanzania (Paediatrc Association of Tanzania-PAT). Kutoka kushoto ni Dr. Augustino Masawe akifuatiwa na Rais wa Chama cha Madaktari wa watoto nchini (PAT) Dr. Rodrick Kisenge, Mrs Jerome na kwa nyuma ni Dr. Francis Furia,Mjumbe na Dr. Hadija Mwamtemi, Mwekahazina wa chama hicho.

Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akifanya mazungumzo na Daktari Bingwa wa Watoto Jerome Paulson kutoka Marekani na Viongozi wa Chama cha Madaktari wa Watoto hapa Tanzania kwenye ukumbi wa mikutano wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo, WAMA, tarehe 21.5.2013. PICHA NA JOHN LUKUWI

JK AONGOZA KIKAO CHA CC YA CCM MJINI DODOMA

Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete akizungumza na wajumbe, wakati wa Kikao Cha Kamati Kuu (CC) ya CCM, kilichofanyika leo May 21, 2013, kwenye ukumbi wa Jengo la White House, Makao Makuu ya CCM mjini Dodoma. Kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa CCM (Zanzibar), Rais wa Zanzibar, Dk. Ali Mohamed Shein na kulia ni Makamu Mwenyekiti wa CCM (Zanzibar), Philip Mangula na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana. (Picha na Bashir Nkoromo)

Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akimkaribisha Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete kufungua kikao cha Kamati Kuu (CC) ya CCM, leo Mei 21, 2013,  kwenye ukumbi wa Jengo la White House, Makao Makuu ya CCM mjini Dodoma. Kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa CCM (Zanzibar), Dk. Ali Mohamed Shein na Kulia ni Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara), Philip Mangula.

Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete na wajumbe wa Kamati Kuu ya CCM, wakiwa mkutano wa Kamati hiyo, leo Mei 21, 2013,  kwenye ukumbi wa Jengo la White House, Makao Makuu ya CCM mjini Dodoma.

Tamko la Msemaji wa Ikulu ya Marekani kuhusu Ziara ya Rais Barack ObamaBarani Afrika

Kuanzia tarehe 26 Juni hadi 3 Julai, Rais Obama na Mkewe wanatarajia kutembelea nchi za Senegal, Afrika ya Kusini na Tanzania. Katika ziara yake hiyo, Rais atawekea mkazo umuhimu ambao Marekani inauweka katika ushirikiano wetu wa kina na unaoendelea kuimarika na nchi za Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara kupitia mipango mbalimbali ikiwemo ile ya kuimarisha ukuaji wa uchumi, uwekezaji na biashara, uimarishaji wa taasisi za kidemokrasia na uwekezaji katika kizazi kipya cha viongozi wa Kiafrika.

Rais atakutana na viongozi mbalimbali wa kiserikali, sekta binafsi na jumuiya huru ya kiraia ikiwemo vijana ili kujadili ubia wetu wa kimkakati katika ushirikano wetu rasmi na masuala mengine ya kimataifa. Ziara hii itadhihirisha dhamira ya dhati ya Rais ya kupanua na kuimarisha ushirikiano kati ya Marekani na watu wa nchi za Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara katika kuimarisha amani na ustawi katika kanda hii na duniani kote kwa ujumla. 

Statement by the Press Secretary on the President’s Travel to Africa

President Obama and the First Lady look forward to traveling to Senegal, South Africa, and Tanzania from June 26 - July 3.  The President will reinforce the importance that the United States places on our deep and growing ties with countries in sub-Saharan Africa, including through expanding economic growth, investment, and trade; strengthening democratic institutions; and investing in the next generation of African leaders.

The President will meet with a wide array of leaders from government, business, and civil society, including youth, to discuss our strategic partnerships on bilateral and global issues.  The trip will underscore the President’s commitment to broadening and deepening cooperation between the United States and the people of sub-Saharan Africa to advance regional and global peace and prosperity.

Kwa Hisani ya Ubalozi wa Marekani Nchini Tanzania

Skylight Band yaanda usiku maalum kwa mashabiki wa Man United kumpongeza Sir Alex Ferguson kwa uongozi uliotukuka

IMG_9111
Model Neema Mbuya akishow love na Mtaalam Sound na dereva wa Skylight Band Ludewa kwenye Bango maalum lenye picha la aliyekuwa Kocha wa timu ya Man United Sir Alex Ferguson ambapo Skylight Band iliandaa usiku maalum wa kumpongeza baada ya kutangaza kustaafu kwa mashabiki wa chama hilo.
IMG_9110
Abby Rasta na Meneja wa Band ya Skylight Aneth Kushaba AK47 wakishow love.
IMG_9120
Mwanadada akibusu picha ya Sir Alex Ferguson kuonyesha mapenzi kwa kocha huyo aliyetangaza kustaafu.
IMG_9123
Mdau mpya wa Skylight Band akishow love kwenye bango maalum la kumshukuru Kocha wa Man United Sir Alex Ferguson baada ya kutangaza kustaafu kwa kuingoza timu hiyo kwa miaka 26 na kuipa makombe 13.
IMG_9125
IMG_9131
Meneja wa Skylight Band ambaye pia ni mwimbaji Aneth Kushaba AK47 akiangusha saini yake kwenye Bango maalum la sherehe ya kumuaga aliyekuwa kocha wa Klabu ya Manchester United Sir Alex Ferguson iliyoandaliwa maalum kwa mashabiki wa timu hiyo jijini Dar.
IMG_9176
IMG_9197
IMG_9199
IMG_9195
Mdau Eric Ndalu naye aliwakilisha.
IMG_9274
Dr. Isack naye alitia saini yake kama shabiki wa chama hilo kubwa lililokuwa likiongozwa na Sir Alex Ferguson.
IMG_9141
Sehemu maalum ya kugawa zawadi kwa mashabiki wa Skylight Band.
IMG_9116
Pichani juu na chini Models wakiwahudumia mashabiki wa timu mbalimbali kwa kuwapa bendera na kuwavisha Rizband hii ilikuwa maalum zaidi kwa mashabiki wa chama kubwa la mashetani wekundu Man United kumtakia kila la kheri Kocha Sir Alex Ferguson baada ya kutangaza rasmi kustaafu ukocha. Juu ni Abby Rasta na chini ni Neema Mbuya.
IMG_9178
IMG_9158
Aneth Kushaba AK 47 akitoa burudani naye ni miongoni Waimbaji bora wa kike wa Band wanaowania Tuzo za Kilimanjaro Music Awards 2013 naye yeye pia anaomba kura wewe Mtanzani ampigie sasa kwa kuandika AM 1 tuma kwenda namba 15345.
IMG_9167
Aneth Kushaba AK47 na Sam Mapenzi wakiwapa raha mashabiki wa Skylight Band.
IMG_9188
Mary Lukas vijana wenzake wakitoa burudani kwa Mashabiki wa Skylight Band....Vijana walipendeza na ubunifu wa aina yake. Mpigie kura Mary Lukas anawania Kili Music Awards 2013 kwenye kategori ya Mwimbaji bora wa kikwe wa Band andika AM4 tuma kwenda namba 15345.
IMG_9207
MAFAHARI WAWILI HAWAKAI ZIZI MOJA....Lakini hawa wameweza....Mdau Chiddo (kulia) akiwa na marafiki zake huku wakiwa wameshikilia bendera za timu wazipendazo katika usiku maalum ambao ulikuwa kimichezo zaidi kwa mashabiki wa Skylight Band.
IMG_9353
Wadau wetu wa Ukweli all the way from New Palm Tree Hotel iliyopo Bagamoyo karibu na Hoteli ya Oceanic iliyoungua Mr & Mrs Braiton Robert (kushoto) wakiwa na mdau anayefahamika kwa jina la Pacha (kulia). Wadau mnakaribishwa kutembelea hoteli hiyo Bagamoyo.
IMG_9245
Mbwembwe za mashabiki wa Skylight Band zilianzia hapo.
IMG_9253
Hapo sasa tenwe kazi.....
IMG_9259
Nderemo na vifijo vililipuka katika ukumbi wa Thai Village.
IMG_9264
Sam Mapenzi wa Skylight Band akiimba wimbo maalum wa mashabiki wa timu ya Man United.
IMG_9292
Asiyekuwa na Mwana aeleke jiwe.....
IMG_9295
Burudani ya Skylight Band ikiendelea ndani ya ukumbi wa Thai Village.
IMG_9297
Warembo wakisakata muziki wa Skylight Band.
IMG_9301
Ebwana Camera hii hapa unatumulika mwanangu cheki basi....Jamaa hana hili wala lile mzuka wa kucheza umemkolea kinoma.....
IMG_9302
Sam Mapenzi wa Skylight Band akicheza na shabiki wake.
IMG_9305
Totoz za ukweli zikiendelea kupagawishwa na uimbaji wa Sam Mapenzi.
IMG_9311
Kila mrembo alitaka kucheza na Sam Mapenzi, kijana machachari asali ya warembo.
IMG_9316
IMG_9332
Asali ya warembo Sam Mapenzi akiendelea kupagawisha mashabiki wa Skylight Band.
IMG_9351
Joniko Flower wa Skylight Band naye ni balaa....cheki wadada wanavyopagawa naye.
IMG_9315
Nyomi ya kumwaga si mchezo...Ni Band inayokuja kwa kasi na kukubalika na watu wa rika zote hapa mujini.
IMG_9328
Burudani mwanzo mwisho na watu wastaarabu ndani ya Thai Village.
IMG_9342
Joniko Flower wa Skylight Band akitoa burudani kwa mashabiki wa Skylight Band.... Anaomba kura yako kama Rapa Bora wa Bendi na Mtunzi Bora wa Mashairi kwenye Kili Tanzania Music Awards tuma neno BG4 au AX3 kwenda namba 15345.
IMG_9355
Shabiki nambari moja wa Skylight Band akijimwaga na sebene lililokuwa likiporomoshwa na Band hiyo.
IMG_9361
Umati wa mashabiki wa Slylight Band ukicheza muziki wa Pwani mduara uliokuwa ukiimbwa na Mary Lukas.
IMG_9365
Usipime wewe Skylight Band ni balaa.
IMG_9372
Mdau Abubakary Abdul na Jembe lake.
IMG_9378
Hemedy a.k.a PHD na Gelly wa Rhymes (kulia) na mdau wakishow love ndani ya Thai Village na Skylight Band.
IMG_9407
Mdau Jacob akishow love.
IMG_9396
IMG_9401